Friday, June 27, 2025

Friday, April 5, 2013

BIBI ALIYE ZALIWA MWAKA 1900 ASIMULIA HAYA:

HADITHI nyingi katika vitabu vya kale husimulia namna binadamu wa zamani alivyoishi miaka mingi, tofauti na ilivyo sasa.
Hata hivyo kuna ukweli katika maisha ya sasa kuwa watu kutoka baadhi ya mataifa wakiwa wamekula chumvi nyingi zaidi na kuingia katika vitabu vya historia.
 Wilayani Mpwapwa kuna mfano mzuri na ambao uko wazi, kwani yuko mwanadamu mwenye umri wa miaka 113 ambaye anaishi hadi sasa na anakula vyakula vyote wanavyokula wengine ikiwemo vitu vigumu kama nyama.
 Ni katika Mtaa Igovu Kitongoji cha Ng’ambo si mbali kutoka katika makaburi ya wakoloni walioishi Mpwapwa zama hizo, katikati ya nyumba nyingi zilizojengwa kwa matofari ya udongo yupo Bibi ambaye ni maarufu kwa jina la Mdala Aksa liyezaliwa mwaka 1900.
 Aksa au Nyamiti (jina la utoto) ni mzaliwa pekee katika familia ya Marehemu Luwaha pamoja na mkewe aliyeitwa Mkaulugu wote wenyeji wa Mkoa wa Iringa, ingawa yeye anapinga kuwa si Iringa bali ni Uheheni.
 Simulizi zinaonyesha kuwa familia hiyo ilikuwa na ukaribu sana na familia ya shujaa na mtemi wa wahehe Mkwawa ambaye ni mtoto wa Muyugumba.
 Bado anaweza kuzungumza na kusikia bila ya shida yoyote lakini kinachomsumbua ni macho kupungua uwezo wa kuona, pamoja na miguu yake kukosa nguvu ingawa anaweza kutembea kwa msaada. Muda mwingi maisha ya mama huyo ni kulala tu.
Ndani ya nyumba
 Nilipoingia ndani ya nyumba nilipata kusikia mambo mengi, kwanza ni historia ya kikongwe huyo ambaye licha ya kupoteza baadhi ya kumbukumbu, anaonyesha mwenye uelewa mkubwa na masikio yake yanasikia kwa ufasaha na umakini wa hali ya juu.
 Simulizi yake
 “Zinji semigwe ninga……”(mengine nimesahau ila…….) anavuta pumzi na kuanza kusimulia kuwa alizaliwa mkoani Iringa baba yake akiwa ni mhehe na mama yake alikuwa ni mgogo mwenye mchanganyiko wa wahehe na alizaliwa akiwa pekee, kutoka kwa mama yake Mkaulugu.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ