Top News
Showing posts with label Vichekesho. Show all posts
Showing posts with label Vichekesho. Show all posts

Thursday, August 1, 2013

Padri, Nitasamehewa kwa hilo, Kama siku Yako haijakaa powa unaweza ukacheki hapa kuiweka powa.

Padri amekaa katika ki-box cha kuungamisha,
kanisani hakuna mtu. Mara muumini mmoja
akaingia,
akapiga magoti upande wa pili na kufanya ishara
ya
msalaba akaanza kuungama.
== "Padri naungama dhambi zangu, leo
nimefanya
dhambi kubwa sana"
"Endelea...."
...
...
== "Bosi wangu aliniita nyumbani kwake
akaniambia amegundua nimeiba shilingi milioni
50,
akasema nisipotoa maelezo ya kutosha
atanipeleka
polisi.
Sasa ukweli mimi naogopa kufungwa na pesa
kweli
niliiba, nikatazama huku na huku nikagundua
tuko wawili peke yetu, nikachomoa bastola
nikamuua.
Nitasamehewa?"
"Utasamehewa...!! " == "Basi wakati nataka
kuondoka nikasikia mlango
unafunguliwa, kutazama loh, mke wa bosi...!!
Akaniuliza nimemfanya nini mume wake.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili
peke yetu, nikamuua na yeye. Nitasamehewa na
hiyo?" "Utasamehewa... "
== "Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke
lakinimlinzi akakataa kufungua geti akasema
amesikia kama kishindo hivi! Nikaona ananiwekea
kiwingu. Kutazama huku na huku nikagundua
tuko
wawili peke yetu nikamuua. Nitasamehewa?"
"Mmm!! Utasamehewa... ."
== "Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda
nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto
wa bosi akabisha hodi nikawaza mambo gani
tena.
Akasema amerudi nyumbani na kukuta
yalotokea,
lakini akanionyesha diary ya baba yake
inayoonesha
kuwa nilikuwa na appointment naye kabla hajafa.
Nikamuuliza nani mwingine anajua, akasema
ameanzia kwangu kisha atakwenda polisi.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili
peke yetu nikamuua. Diary nikaichomamoto.
Nitasamehewa na hilo?"
Kimya........ "Padri, Nitasamehewa kwa hilo?"
Kimya.........
Jamaa kutazama kwenye kibox padri hayupo.
Lakini kwenye kona moja akaona kabati la ngou
za
mapadri kama linatikisika.
Kufungua akamuona Padri kajificha katikati ya
majoho anatetemeka.... .
"Sasa baba mbona umenikimbia?"
Padri kwa taabu akajibu...
"Nilitazama huku na huku nikagundua kuwa tuko
wawili peke yetu........"
Read more ...

Wednesday, July 31, 2013

Kama siku yako ya leo haijakaa poa Cheki hapa Kuifanya siku yako iwe poa....!

Jamaa fulani alikuwa na
tabia ya kujamba kwa
nguvu kila aamkapo
asubuhi. Mkewe alikerwa
sana na tabia hiyo,
alimkataza akachoka, siku
moja akamwonya kuwa iko
siku badala ya ushuzi,
utumbo utakuja kumtoka.
Jamaa alicheka sana
kusikia hilo. Siku moja
mke alilazimika kuamka
alfajiri awatengeze kuku
kwa ajili ya sherehe,
alipowatoa utumbo wale
kuku akakumbuka
alichowahi kumwambia
mumewe akaamua
kumtisha, akamnyatia
mumewe ambaye alikuwa
bado amelala na
kumuwekea utumbo
kwenye pajama lake na
kurudi jikoni. Muda si
mrefu mwanaume aliamka
akajamba kwa nguvu kama
kawaida yake, lakini
akahisi kitu cha baridi
ndani ya suruali, ile
kuvuta si akakuta utumbo.
Akapiga ukelele,’Mama
yangu nimekufa’. Mke
wake aliposikia akacheka
peke yake, akajua jamaa
kashaukuta ule utumbo.
Kimya cha kama nusu saa
kilipita. Hatimaye jamaa
akamfuata mkewe jikoni
akiwa amelowa jasho
pajama nzima.
JAMAA: Mke wangu yale
uliosema leo yametokea.
MKE: Yepi jamani?
JAMAA: Mke wangu
ulisema nikiendelea
kujamba utumbo utatoka,
leo utumbo si umetoka
kama ulivyosema
MKE: Pole mume wangu,
sasa?
JAMAA: Namshukuru
Mungu, nimejitahidi
nimeusindilia na vidole na
nimeweza kuurudisha
ndani wote.
MKE: Mungu wangu
umefanyaje?
Read more ...

Sunday, July 28, 2013

Ha ha ha Dah Mbavu zangu! Kama jumapili yako haijakaa powa basi Unaweza Cheki hapa

Mtoto: Baba nitumie hela ya matumizi huku shule hali ni mbaya la sivyo nitajinyonga.
Baba: Huku nyumbani hli ni mbaya kuliko huko shuleni, kwa hiyo kama unajinyonga sawa tu kwa sababu utapunguza bajeti. Kopa kamba dukani ntakuja kulipa nikija kuchukua maiti yako. Mungu akulaze mahali pema peponi mwanangu.

 MC anamsifia Bi. Harusi
"Sasa nawapa sifa kubwa ya Bibi harusi. Tangu namfahamu huwa havai nguo za ndani!"
Watu wakaduwaa
MC "Narudia tena kwa msisitizo na sijakosea. Bi. Harusi huyu huwa havai kabisa nguo za ndani. Yeye anavaa za kutoka Italy, England na USA. Si za Tanzania. Hebu mshangilieni!"
Kila mtu "Ahaaaaaa...!"

 MPARE NA PESA
Binti: Mama, nimemuomba baba hela ya saluni akaninyoa nywele
Mama: Una bahati sana mwanangu. Ungemuomba hela ya whitedent angekung'oa meno!

 UWONGO HAUFAI
Jamaa: Unasoma?
Demu: Hapana sisomi, vipi wewe unasoma?
Jamaa: Ndo nipo form 4 Jangwani
Demu: Jamani hiyo si shule ya wasichana?
Jamaa: Ah! sorry nimechanganya nipo Kisutu
Demu: Mwee mbona nayo ya wasichana
Jamaa: Haa! Nilikuwa nakutania nachukua PhD IFM
Demu: Mh! Ina maana IFM imeanza kutoa PhD?
Jamaa: Ishia zako. Demu mwenyewe hulipi wala nini! Unauliza maswali kama tupo uhamiaji? KWA TAARIFA YAKO NACHUKUA DEGREE YA UDAKTARI CBE!

 Mlevi kaanguka toka ghorofani fasta watu wakamfata kumsaidia wakamuuliza VIPI IMEKUAJE? Mlevi akajibu: "HATA SIJUI NA MIE NDO NAFIKA SASA HIVI..."


Read more ...

Wednesday, July 24, 2013

Kama siku yako ya leo haija kaa Poa Cheki hapa.. Ha ha ha!

(Joni) dogo wa darasa la kwanza kafika shule akaanza kulalamika kwa mwalimu wake wa darasa kwamba la kwanza si saizi yake na anataka arushwe hadi darasa la tatu kwa maana anaamini ana akili kumzidi hata dada yake ambaye yuko darasa la tatu. Ticha wa darasa kuona dogo kazidi kupiga kelele na kusumbua akamchukua akaenda naye kwa mwalimu mkuu. Ticha wa darasa: Huyu mtoto hata simuelewi, darasani anapiga kelele kwamba anataka apelekwe na darasa la tatu kwamba la kwanza si saizi ya akili zake.

Ticha mkuu akapigwa: Ngoja nimuulize maswali ya la tatu akishindwa arudi darasani na akae atulie vinginevyo acheze na bakora. We mtoto, tatu mara tatu ngapi?
Joni: Tisa mwalimu.
Ticha mkuu: Tisa mara 4?
Joni: 36
Basi ticha mkuu akamkandamiza dogo maswali kibao ya darasa la tatu dogo akawa anapatia.
Ticha mkuu: mwalimu mi naona kijana yuko sawa, hebu mpeleke tu darasa la tatu, fanyeni utaratibu wa kumuingiza kwenye atendensi ya darasa la tatu.
Ticha wa darasa: sawa mwalimu ila ngoja nimuulize maswali zaidi. Joni ni kitu gani ambacho ng'ombe anavyo vinne na mimi ninavyo viwili?
Joni: Miguu
Ticha: Kitu gani unacho ndani ya kaptula yako ya shule ambacho mimi sina? (Ticha mkuu akashtuka kuhusu hilo swali)
Joni: Mifuko
Ticha: Kitu gani mbwa anakifanya halafu binadamu anakikanyaga?
Joni: Kujisaidia haja kubwa njiani. (ticha mkuu mdomo ukawa uko wazi anashangaa)
Ticha: Kitu gani ukikiingiza ndani kinakuwa kigumu na cha rangi kama nyekundu au pink lakini kikitoka kinakuwa kilaini na kinanata nata? (Ticha mkuu jicho likamtoka lakini kabla hajamzuia dogo kujibu dogo akatoa jibu)
Joni: Big G.
Ticha: Kitu gani mwanaume anakifanya akiwa amesimama, mwanamke akiwa amekaa na mbwa akiwa kasimama kwa miguu mitatu?
Joni: Kujisaidia haja ndogo.

Ticha mkuu akaanza kutetemeka.

Ticha: Neno gani linaanza na herufi K na linaishia na herufi A ambalo huleta raha sana watu wakilitamka?

Joni: KULA

Ticha mkuu akavuta pumzi ndefu halafu akazishusha akasema: Mwalimu naona mpeleke Joni darasa la tano. Maswali yote sita ya mwisho mimi mwenyewe nimekosea majibu yake.
Read more ...
Designed By ApexbnewZ