Bunge limefikia uamuzi huo juzi kwa kupiga kura za
sauti, kupinga hoja ya Msemaji wa Kambi wa Upinzani katika Ofisi ya
Rais (Utumishi), Profesa Kulikoyela Kahigi.
Profesa Kahigi alitaka Bunge liitake Serikali
kuchunguza tuhuma hizo na kuwachukulia hatua watuhumiwa hao, suala
ambalo liliibua mvutano baina ya Kambi ya CCM na Serikali kwa upande
mmoja na upinzani kwa upande mwingine.
Mvutano huo ulitokea juzi wakati Bunge limekaa kama kamati kupitisha kifungu cha mshahara wa Waziri.
Profesa Kahigi alisema kambi yake imetoa tuhuma
dhidi ya maofisa usalama wa taifa, kuwatesa watu na kutumika kupanga
njama, lakini Serikali imekaa kimya bila kuchukua hatua dhidi ya tuhuma
hizo.
“Ninachoomba ni kitu kidogo tu, hoja yangu hapa ni
kwa nini Bunge na Serikali havichukui hatua, ninatoa shilingi mpaka
mtakapoeleza ni hatua gani mtazichukua dhidi ya tuhuma hizi,” alisema
Profesa Kahigi.
Suala hilo lilizua mjadala na kusababisha Waziri
wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kusema Bunge siyo sehemu ya
mashtaka na kwamba, kama kambi hiyo inazijua tuhuma hizo izipeleke
polisi huko ndiyo hatua zitachukuliwa.
“Nendeni polisi mpatiwe RB (Kumbukumbu ya taarifa
polisi) halafu tuhuma zitafuatiliwa. Hatuwezi kwenda kuwashughulikia hao
watu mnaowasema,” alisema.
Chikawe.
Awali, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George
Simbachawene alisema tuhuma hizo kisheria zinatakiwa zipelekwe polisi
siyo bungeni.
“Hatuwezi tukashughulikia tuhuma kwa kuwa tu
mmesema kwamba tuzichukulie hatua,.Naomba wanasheria wenzangu tufuate
sheria kwa kuwa tunazijua,” alisema Simbachawene.
Hata hivyo, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema)
alipinga hilo na kwamba, kazi ya Serikali ni kuchukua hatua dhidi ya
tuhuma zinazotolewa bungeni na mahali pengine siyo kuzungukazunguka.
No comments :
Post a Comment