Top News

Monday, April 29, 2013

KutokaBUNGENI: ANNA MAKINDA AWASIFU CHADEMA BUNGENI

Ni wakati wa kuahirisha kikao cha leo asubuhi dakika tatu zilizopita.

Kulikuwa na msuala matatu yaliyojitokeza bungeni moja la Waziri kuja bungeni na kutoa kauli ya serikali kwa mdomo bila kuwa na maandishi kama inavyotakiwa na kanuni.

Suala jingine ni la mabadiliko ya utaratibu wa kupitisha vifungu bunge litakapokaa kama kamati. Maswali kuhusu hili yalijikita kwenye ukweli kwamba hakuna document yoyote iliyoletwa na hivyo itakuwa hawajui ni kifungu kipi kinapitishwa na hivyo serikali irudi tena ije na documents kama inavyotakiwa.

Swali la Waziri kutokuja na document liliulizwa na Zitto Kabwe na baaday msisitizo ukawekwa na Tundu Lissu kwa kutaja kanuni 49(3) isemayo hivi: {Waziri mwenye kutoa kauli atawajibika kutoa nakala ya kauli yake kwa Wabunge wote wakati anapoiwasilisha Bungeni.}

Wakati swali la serikali kutakiwa kuja na document kwa ajili ya Kamatiya matumizi liliulizwa na John Mnyika.

Spika alipoinuka alikubaliana na swali la kwanz akwa Waziri kwamba waliamua Waziri aje kwanza atoe kauli ya mdomo lakini himazuii kutoleta statement na hivyo atahitajika kuileta ili isiishie kuwa ya mdomo.

Kuhusu swali la Mnyika, Spika alisema lilikuwa ni swali obvious na angeshangaa kama wabunge wasingeuliza. Na akataja kwamba sababu ni kwamba utaratibu huu ndio mara ya kwanza unatumika na hivyo estimate ya muda ilifanya ifanyike hivyo. Lakini amekiri kwamba kabla ya kukaa kama kamati ni lazima watoe documents watakazogawiwa wabunge.

MY TAKE:

Tumeona Spika akisema kuwa angeshangaa kuona kama wabunge wasingeuliza maswali hayo ya msingi. Pia amekubaliana nao. Lakini wasingeuliza ili kutimiza mshangao wake basi hatujui ingekuwaje na huenda ingekuwa kama ilivyoelekea kuwa.

Sasa, kama Spika alijua kuwa haya ni maswali ya msingi na ya kikanuni, hebu angalia walioyauliza (Zitto, Tundu, Mnyika). Wote ni Chadema.

Utaachaje kusema kwamba alichotarajia hoja y amsingi kama ile isiulizwe na wabunge kwa kweli kwa namna moja ni sawa na yeye kujua kwamba haiwezekani hoja ya msingi ipite kimya mle bila Chadema kuuliza.

Hakuna CCM hata mmoja aliyeinuka kusema lolote katika haya ambapo yasingesemwa yangepita hivihivi tu kama ilivyoelekea.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ