Top News

Friday, April 5, 2013

MTANZANIA ALIYEFIA CHINA NA MAITI YAKE KUHIFAZIWA HOSIPTALINI HUKO MWAKA MZIMA:

MFANYABIASHARA, Mkumbukwa John Shayo (37)  (pichani) aliyefariki katika kifo chenye utata nchini China amezikwa Jumatano iliyopita na kulifanya Jiji la Mwanza kutawaliwa na majonzi.
 
Baadhi ya waombolezaji wakitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lililobeba mwili wa marehemu Mkumbukwa Joseph.
Umati wa watu ulihudhuria mazishi hayo nyumbani kwa bibi wa marehemu, Mabatini kisha kuelekea katika Makaburi ya Buzuruga, Nyakato na kila mtu alionekana kujawa na huzuni.
Hata hivyo, mazishi hayo yaliathiriwa kidogo na mvua iliyofanya baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki washindwe kuuaga mwili wa marehemu.
 
Watu wakipita kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Josephat Mkumbukwa. Kushoto ni mjomba wa marehemu Erasto Kombe.
Mkumbukwa alifariki China na maiti yake kuhifadhiwa hospitali kwa takriban mwaka mzima na serikali ya nchi hiyo huku mkewe, Neema Majukano pamoja na rafiki wa marehemu aitwaye Haji Msongore wakilaumiwa kwa kushindwa kutoa taarifa mapema juu ya kifo hicho.
 
Paroko wa Kanisa Katoliki Kigango cha Mabatini Nyamagana, Charles Bundu, akiendesha ibada ya kuuombea mwili wa marehemu Joseph Mkumbukwa aliyeuwa nchini China mwaka jana. 
Aidha, utata umegubika kifo cha Mkumbukwa kufuatia rafiki huyo wa marehemu ambaye mara ya mwisho walikwenda wote nchini Chini kudaiwa kumuoa mke wa marehemu, Neema.
 
Marehemu Joseph Mkumbukwa enzi za uhai wake.
 
Dada wa marehemu akisaidiwa na waombolezaji mara baada ya kuuaga mwili wa marehemu kaka yake.
Source GPL

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ