Barua pepe ya Dr. Asha-Rose Migiro inasema: “Naandika kuhimiza kazi ya
kuwatia hamasa Makatibu wa Mikoa wasimamie kikamilifu mchakato wa
kuundwa kwa Mabaraza ya Wilaya ya Katiba. Kama mnavyofahamu Tume ya
Katiba imeshatoa taarifa rasmi kwenye vyombo vya habari ... kuhusu zoezi
hili muhimu. Sambamba na hatua za awali tulizochukua baada ya kupata
rasimu ya mwanzo ya Mwongozo wa Tume, hivi sasa tunatakiwa tuongeze
juhudi za ushiriki wetu na kutayarisha makundi husika kama
tulivyokwishaongea.”
Baada ya kuagiza ‘mawasiliano kati ya SUKI na Makatibu wa Mikoa’ kuhusu
mambo ya kufanya, Dr. Asha-Rose Migiro alimalizia barua yake kwa maneno
yafuatayo: “Tafadhali wanakaliwa msisite kutoa maoni, ushauri na mbinu
bora zaidi za kutimiza azma yetu katika suala hili muhimu.” ‘Wanakiliwa’
wa barua pepe ya Dr. Asha-Rose Migiro ni pamoja na Mh. Mwigulu Nchemba,
Mh. Zakhia Meghji, Mh. Muhamed Seif Khatib na Bw. Nape Nnauye, Katibu
Mwenezi wa NEC ya CCM.
Siku moja baadaye, Nape Nnauye aliwaandikia ‘wanakiliwa’ wenzake kama
ifuatavyo: “NASHAURI ikiwezekana kwa sababu ya unyeti wa swala hili
tupate taarifa kila siku/au walau siku tatu ya HALI HALISI inavyoendelea
katika kila mkoa, ni vizuri idara ikaandaa checklist ya mambo muhimu ya
kupima kama mchakato unakwenda vizuri au la! Mfano ... idadi ya
walioandaliwa kugombea katika kila eneo, idadi ya waliohamasishwa
kuhudhuria na kupiga kura, n.k.”
Mnamo tarehe 18 Desemba mwaka jana, Katibu wa Sekretarieti ya
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Francis K. Mwonga, aliwaandikia barua
Makatibu wote wa CCM wa Mikoa kuwapa ‘Maelekezo ya Kikao cha
Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa na Makatibu wa CCM wa Mikoa
Kilichofanyika Dar es Salaam Tarehe 10/12/2012.’
Sehemu ya Maelekezo hayo inasema: “Wakati wa kupiga kura ya maoni kuhusu
Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mawasiliano yafanywe na
wahusika ili vituo vya kupigia kura visiwe mbali sana na wananchi.”
Maneno haya yameandikwa hata kabla Tume haijamaliza zoezi la kukusanya
maoni ya wananchi na tayari Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM
inawaelekeza makada wake mikoani kufanya mawasiliano na ‘wahusika’ juu
ya namna ya kupanga vituo vya kupigia kura.
Mawasiliano haya ya viongozi wa ngazi za juu za CCM yanathibitisha
kwamba mchakato wa Katiba Mpya umeiingiliwa na kuhujumiwa kwa kiasi
kikubwa na CCM. Aidha, mawasiliano haya yanathibitisha kauli iliyotolewa
mbele ya Bunge lako tukufu na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani
Bungeni wakati wa mjadala wa hoja ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwamba
“...viongozi wa kiserikali kama vile Wakuu wa Wilaya na wa Mikoa
waliwahamasisha wenyeviti wa vijiji, mitaa na madiwani kuhakikisha
kwamba wagombea wote wasiokuwa wa CCM, hasa wa CHADEMA, wanaenguliwa
katika chaguzi za vijiji, mitaa au kata.” Aidha, mawasiliano haya
yanathibitisha kauli ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwamba Mabaraza
ya Katiba ya Wilaya yaliyochaguliwa kwa utaratibu “...ni mabaraza ya CCM
na sio mabaraza ya katiba ya Watanzania wote.”
hawa watu hawana lengo zuri na Taifa.kama wananchi wasipokua makini Taifa linakwenda kuangukia mikononi mwa kundi la watu wachache wasio na uzalendo kwa nchi yao.Hata hivo hakuna lisilo na mwisho pamoja na mbinu zao zote watu wamefunguka na hawatafanikiwa.
ReplyDelete