Top News

Thursday, May 2, 2013

MCHUNGAJI MSINGWA CHADEMA APOKEA MESEJI ZA VITISHO KWA KUSHLIKILIA BANGO SUALA LA TEMBO

Mchungaji Msigwa katika uchangiaji katika kikao cha Asubuhi ameongea kwa uchungu sana kuhusu jinsi rasilimali za nchi hii zinavyoteketezwa kwa manufaa ya watu wachache.Ameshangazwa sana na Kitendo cha waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dr. Nchimbi kwa kuendelea kutetea ujangili kwa ngonjera baadala ya kumtaka Msigwa alete ushahidi ili yeye kama waziri aliyepewa zamana kuchukua hatua stahiki kwa watuumiwa.Ila ashangai Coz Nchimbi alianza kuitwa Dr. kabla ya kuwa Dr.

Kuhusu Mgogoro wa Loliondo anasema inashangaza Waziri anateuliwa na Raisi,Katibu Mkuu wa CCM anateuliwa na Raisi iweje jambo ambalo limetolewa uhamuzi na waziri likachunguzwe na hao wateule wengine wao Rais? Hili linaonyesha udhaifu katika taasisi ya Raisi.

Uwezo wa CCM kutataua mgogoro huu ni mdogo sana kwasababu wao ndiyo waliutengeneza tangu enzi za mwinyi.Baada ya yeye kusoma hotuba yake amekuwa akipokea simu(Private Number) zikimtisha kwa kushikia bango issue ya Tembo.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ