Top News

Saturday, May 25, 2013

RAMA MLA WATU AACHIWA HURU

Mshtakiwa Ramadhan Selemani Mussa, maarufu kama ‘Rama mla vichwa’, aliyekutwa na kichwa cha mtoto kikiwa bado kinavuja damu, pamoja na mama yake Hadija Ally, wameachiwa huru.
Rama na mama yake walikuwa wakikabiliwa na shtaka moja la kumuua kwa makusudi mtoto Salome Yohana (3), kinyume cha kifungu cha 196 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).
Hata hivyo, jana Mahakama Kuu ilimwachia huru Rama baada ya kuridhika na ripoti ya jopo la madaktari waliomfanyia uchunguzi wa akili yake, iliyoeleza kuwa wakati wa tukio hilo hakuwa na akili timamu.
Wakati Rama akiachiwa kwa kutokana na ripoti hiyo ya madaktari, mama yake aliachiwa huru baada ya upande wa mashtaka (Jamhuri) katika kesi hiyo namba 26 ya mwaka 2010, kudai kuwa hauna nia ya kuendelea kumshtaki.
Kuachiwa kwa washtakiwa hao kulisababisha vilio kwa mama wa mtoto aliyeuawa, Upendo Dustani na shangazi wa mtoto huyo, Furaha Mussa, aliyekuwa akiishi na mtoto huyo nyumbani kwake Tabata.
Septemba 29, 2011, Mahakama Kuu iliamuru Rama apelekwe katika hospitali ya magonjwa ya akili ili apimwe akili kama alikuwa na akili timamu au la, wakati wa tukio hilo.
Amri hiyo ya Mahakama iliyotolewa na Jaji Samuel Karua, ilitokana na maombi yaliyotolewa na Wakili Yusuph Shehe aliyekuwa akiwatetea
Wakili Shehe alisema ameamua kutoa ombi hilo ili kujiridhisha na utimamu wa akili za mshtakiwa kwanza kabla ya kuanza usikilizwaji wa kesi hiyo kulingana na kumbukumbu za maelezo ya ushahidi ulioko mahakamani.
Jana, kabla ya washtakiwa hao kuachiwa, Wakili wa Serikali, Secy Mkonongo aliyekuwa akisaidiana na Clara Charles, alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali, kwa ajili ya kuwasomea maelezo ya awali washtakiwa hao.
Hata hivyo Wakili Shehe alidai kuwa mara ya mwisho Mahakama hiyo iliamuru mshtakiwa wa kwanza, Rama, apelekwe katika hospitali ya magonjwa ya akili kwa ajili ya uchunguzi wa akili yake.
Wakili Shehe alisema ripoti hiyo tayari imeshawasilishwa mahakamani hapo kutoka Taasisi ya Magonjwa ya Akili Isanga tangu Juni 20, 2012, ikiwa imesainiwa na Dk Mndeme Erasmus na kwamba inaeleza kwa mshtakiwa wakati akitenda kosa hilo hakuwa na akili timamu.
“Kutokana na ripoti hii, ninaiomba Mahakama yako ijielekeze katika vifungu cha 220 (4) na 219 (2) vya CPA kinachoelekeza Mahakama

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ