
Hivi karibuni zimefanyika juhudi kubwa kunusuru wasanii kutumbukia
katika umaskini wa kutupwa dhidi ya makampuni ya simu kunyonya kazi zao
na upande wa pili baadhi ya radio ambazo zinaonesha upendeleo ,
unyanyasaji na unyonyaji wa wazi kwa kazi za wasanii.Clouds FM hivi
karibuni imeshutumiwa na Lady Jay Dee kuendesha kampeni za kumuua
kisanii ambapo pia imewalipa baadhi ya wasanii ambao walitakiwa
kuhudhulia show ya Lady JayDee ili wasitokee katika shoo hiyo.Jamii
haipendezwi na vita hii japo serikali imeonekana kufumba macho na
kujifanya haioni kinachoendelea.Tuko pamoja katika kuona haki,usawa na
amani vinatendeka.Mungu Ibariki Tanzania
No comments :
Post a Comment