Top News

Thursday, September 26, 2013

Irene Paul ajiona mwenye bahati baada ya kupata nafasi ya KUTOMASWA na Van Vicker ambaye ni staa wa Nigeria



Msanii wa sinema za Kibongo, Irene Paul amesema ameridhishwa na uwezo wa
mkali wa sinema za Kinigeria, Joseph Van Vicker akidai ni jasiri na
mjuzi sana katika scene  za mapenzi.

Akizungumza na mwandishi wetu, Irene alisema kuwa pamoja na kuigiza naye kwa mara
ya kwanza ‘scene ya on bed’ lakini Vicker alionesha uzoefu wa hali ya
juu utadhani wanafahamiana kitambo, jambo lililomshangaza na kujikuta
akiingiwa na woga.

  “Jamaa utadhani tunafahamiana, alinikabili
kitandani kwa kiwango kikubwa sana, nilipata hofu kubwa mno. Van anajua
kuigiza jamani, kwangu hii ni bahati ambayo namshukuru Mungu kuipata,
wengi waliililia,” alisema Paul.
 
Van aliibuka Bongo na kuondoka wiki
iliyopita kwa ajili ya kushuti sinema moja na wasanii wa nyumbani
ambayo bado haijapatiwa jina.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ