Top News

Saturday, October 12, 2013

Picha na Video: Mtindo mpya wa Burudani ndani ya New Maisha Club wasababisha Snura Kudondoka Stejini Akikata Mauno.

New Maisha Club 1Usiku wa October 11 2013 New Maisha Club Dar es salaam imeleta kitu kipya kwa Watanzania, ubunifu wao mwingine sasa hivi ni disco linalopigwa na Band kama inavyofanyika kwa baadhi ya nchi zilizoendelea.
Hii yote ni kuleta utofauti lakini wenye nguvu na utakaoleta shangwe zaidi kwa kila anaetia mguu Maishani ambapo kazi inapigwa na Dvj Majay kwenye mashine alafu Zungu Mnyama akawa anamiliki drums, kiufupi ni kwamba Zungu kazi yake kubwa ni kufatilizia nyimbo zinazopigwa na Majay kisha yeye anazigonga kwa ujuzi wa drums.
Unaweza kuchek video za hii style mpya Tanzania ambayo pia itaonyeshwa kwa wakazi wa Mtwara Jumamosi hii ya October 12 2013.
New Maisha club 2
New Maisha club 3
new maisha club 4

Kwenye hii video ya mwisho Snura ambae ni staa wa single za ‘Majanga’ na ‘nimevurugwa’ alionekana kwenye stage akionyesha ujuzi wake kwenye kukata viuno alafu mwishoni kwa bahati mbaya akaanguka wakati anataka kukinogesha..


Na Millard Ayo

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ