Top News

Wednesday, August 6, 2014

Picha: AY ,D'Banj, Fall Ipupa wametembelea makao makuu ya benki ya dunia jijini Washington DC

Rapper Ambwene Yessaya aka AY aiwa na wasanii wenzake wa mradi wa One Campaign, jana wametembelea makao makuu ya benki ya dunia jijini Washington DC, Marekani.



Fally Ipupa, AY na D’Banj




AY aliongaza na D’Banj, Fally Ipupa na wengine.


“Kwanza jana tulikutana na wajumbe wa Youth African Leadership Initiative wale ambao walichaguliwa wakaja hapa kama miezi miwili hivi ambao kwa Tanzania kwa haraka haraka niliwaona ni mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari, Naibu waziri wa Nishati na Madini Steven Masele hao wawili niliwaona na watu wengine wa serIkali ya Zambia pamoja na viongozi mbalimbali wa nnchi za Afrika,” AY ameiambia Bongo5.


“Baada ya kukutana nao hapo sisi tukaenda kwenye rehearsal na introduction na baada ya hapo tukafanya rehearsal pamoja na wasanii wa Afrika ambao walikuja nahisi tulikuwa wasanii tisa au nane kwa sababu hatukuja wasanii wote ambao tulifanya ile project ya wimbo. Baada ya kumaliza ile function ambayo ilikuwa inafanyika white house watu wakaja kwenye ukumbi ambao ulikuwa unaitwa Newseum ambapo tukafanya kama after party tuka perform. Ilikuwa nzuri sana honestly,” ameongeza AY.


“Kwahiyo tukapiga fresh show nzuri sana, watu walifurahi sana. Tuliperform wimbo mmoja mmoja. Tukaperform mimi na Mwana FA, tukafanya Bila Kukunja Goti, tuliwachezesha mpaka wazee wazee ambao wapo kwenye serikali. Baada ya hapo tukaperform pamoja wimbo wa Cocoa na Chocolate then baada ya hapo ngoma ikawa imeisha. Leo (jana) hapa najitayarisha tunaenda World Bank na baada ya kwenda world bank halafu tutaenda Capital Center pia tutakuwa na meeting na watu ambao wana uhusiano na white house kwaajili ya kupitisha haya mabilioni kama ambavyo unaona wanayatoa kwenye CNN, Aljazeera na baada ya hapo kunaweza kukawa na after part nyingine I think baadaye kwaajili ya kuangana halafu kesho (leo) kila mtu anaweza kurudi kwake,” amesema.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ