Rapper Fat Joe jana (August 26) alitweet ujumbe wa kuwaaga mashabiki wake kabla ya kwenda mwenyewe kuripoti jela ya Federal Detention Center, Miami , Marekani kuanza kutumikia kifungo cha miezi minne jela alichohukumiwa baada ya kukutwa na hatia ya kushindwa kulipa madeni ya kodi.
![FAT-JOE (1)](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_tHPfcuP3cfSCQ4BsIbzzShEJsZ6SJzd_z0qrulVuY3JG_TSuM69fGdEDp1FfC2OYWnTBVOKVHPHfyD7BoG9isqSNZ14sJuq70QGSxuSmcdO3KXj2tveu70qkPJt_yI1XkZ=s0-d)
Joseph Cartergena a.k.a Fat Joe alitweet, “FARE WELL MY PEOPLE IM BOUT TO TAKE THAT RIDE SEE U AT DIDDYS HOUSE FOR NEW YEARS#GODWILLINGINSHALLAH,”
Fat Joe hakuondoka hivi hivi bali aliamua kuwaachia mashabiki wake zawadi ya mixtape yake ‘The Darkside Vol. 3’ bure.
Fat Joe (June 24) alihukumiwa kifungo cha miezi 4 jela baada ya kushindwa kulipa madeni ya kodi (income taxes) zaidi ya $ 1 million kwa kipindi cha miaka miwili 2007 na 2008.
Kifungo hicho kinaambatana na faini ya $15,000 pamoja na usimamizi maalum wa mwaka mmoja baada ya kutoka jela.
No comments :
Post a Comment