UIMBAJI stadi wa Wibo wa YAHAYA wa Nguli
wa muziki wa Kizaki kipya Lady Jay Dee umemjaza mahela Msanii wa Filamu
aliyejizolea umaarufu kwa miaka ya hivi karibuni, Elizabeth Michael
‘Lulu’ wakati akiimba wimbo huo na Jide wakati wa uzinduzi wa Video yake
mpya na yakwanza kusimama peke yake ya FOOLISH AGE.

MSANII wa Filamu Bongo,
Elizabeth Michael 'Lulu', usiku wa kuamkia leo amefanikisha zoezi la
uzinduzi wa filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Foolish Age .
Baada ya move hiyo kali ya dakika 120
iliyooesha ukali wa staa huyo kuoneshwa kwa dakika 20 tu na kubakisha
zingine 100 kusubiri wateja kuziona majumbani kwao alipanda jukwaani
kujitambulisha na kutoa shukrani kwa wamepenzi wa tasnia ya filamu
nchini Tanzania kwa muitikio wao alipanda na kuimba wimbo huo wa Yahaya.
Akianzia kuimba kiitikio cha wimbo huo
akiwa Back Stage, Lulu aliwashangaza watu pale alipomudu vyema wimbo huo
kiasi cha mashabiki ‘Mapedeshee’ wakiongozwa na Pedeshee Rich Rich,
kupanda jukwaani na kumtunza fedha kibao ambazo hakika zilimpagawisha
msanii huyo na mwisho wa wimbo huo alisema mziki unalipa.
Tukio
la uzinduzi huo lilifanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, na
kuhudhuriwa na mastaa kibao wa tasnia mbalimbali hapa Bongo, wakiwemo;
Judith Wambura 'Lady Jaydee', ambaye alitumbuiza sambamba na Barnaba na
Amini.
Wasanii mbalimbali walihudhuria show hiyo usiku huu pale Mlimani City
Lulu
akizungumza machache mara baada ya Move yake hiyo kuoneshwa kwa
mashabiki na wapenzi wa filamu Tanzania ndani ya Ukumbi wa Mlimani City.
Wadau walifuatilia burudani...
Jide akikamua jukwaani...
Mama na mwanao ni kama chanda na Pete... huyo ni Natasha (kulia) na Bintiye Monalisa.
.... Walitunzana tu kivyao vyao...
noti alizo tuzwa
Rich Rich akimwaga noti
Wadau wakifuatilia uzinduzi huo wa Filamu.
Furaha ilitawala
Mwogozaji wa Filamu za Kibongo, Leah Mwendamseke nae alikuwepo kuangalia kazi hiyo ya Lulu.
Waongoza Shughuli hiyo watangazaji wa Redio na TV Double G na mwana dada kutoka Times FM walikuwepo.
Baada ya move hiyo kali ya dakika 120
iliyooesha ukali wa staa huyo kuoneshwa kwa dakika 20 tu na kubakisha
zingine 100 kusubiri wateja kuziona majumbani kwao alipanda jukwaani
kujitambulisha na kutoa shukrani kwa wamepenzi wa tasnia ya filamu
nchini Tanzania kwa muitikio wao alipanda na kuimba wimbo huo wa Yahaya.
Akianzia kuimba kiitikio cha wimbo huo
akiwa Back Stage, Lulu aliwashangaza watu pale alipomudu vyema wimbo huo
kiasi cha mashabiki ‘Mapedeshee’ wakiongozwa na Pedeshee Rich Rich,
kupanda jukwaani na kumtunza fedha kibao ambazo hakika zilimpagawisha
msanii huyo na mwisho wa wimbo huo alisema mziki unalipa.
“Jamanieee kumbe mziki unalipa ile mbaya
yaani nimeimba ubeti mmoja tu hapa ona hela kibao, kuanzia sasa na
mimi nitaanza kuimba mziki”, alisikika Lulu akisenma huku akishangiliwa
na mashabiki wake.
Read more ...