Top News

Saturday, September 28, 2013

Picha: Hawa ndio wahukumiwa wa EPA walio hukumiwa kwenda Jela.


Washtakiwa watatu kati ya watano waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wamehukumiwa kifungo jela baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwatia hatiani ambapo kati yao ni mke na mume. Kushoto ni Bahati John amehukumiwa kifungo cha miaka 7 na katikati ni Manase Mwakale amehukumiwa miaka 5 na mkewe Eddah Mwakale amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja.

Manase Mwakale akiongea na wakili wake baada ya kuhukumiwa kifiungo cha miaka mitano jela.
Eddah Mwakale akiongea na wakili wake. Kulia ni Mume wake, Manase Mwakale ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela.
Washtakiwa wakitoka mahakamani baada ya kusomewa hukumu yao.

No comments :

Post a Comment

Designed By ApexbnewZ